PlaneteAfrique
Déconnexion

WS-Apps, Le système de gestion de contenu adaptatif développé depuis 15 ans est conçu pour sa puissance son efficacité et sa simplicité. WS-MySite! pour votre présence web immédiate, WS-Webzine pour vos publications, Ws-Ecommerce pour votre business.

Watanzania waombwa kutunza amani

Publié le 12/17/2012
Watanzania waombwa kutunza amani


Viongozi na wafanyakazi wa mashirika mbalimbali walioshiriki kuwarejesha kwao wakimbizi wa Burundi waliokuwa wakihifadhiwa katika kambi ya Mtabila wilayani Kasulu wamewaomba watanzania  kujiepusha na vitendo vinavyoweza kuvuruga amani hapa nchini.



Wakizungumza baada ya kukamilisha kazi ya kuwarejesha kwao wakimbizi wa Burundi wamesema kuwa maisha ya ukimbizini waliyoyashuhudia ni ya shida na ghadhabu nyingi, hivyo watanzania wanapaswa kuhakikisha kuwa amani iliyopo  nchini haipotei.



Baadhi ya viongozi wa serikali na wafanyakazi wa  mashirika ya kitaifa na kimataifa wameshuhudia familia ya mwisho ya mkimbizi wa Burundi akipanda basi kurejea kwao.



Hata hivyo pamoja na mafanikio ya kukamilisha kazi ya kuwarejeshwa kwao zaidi ya wakimbizi elfu 35 kabla ya muda uliopangwa walikabiliwa na changamoto mbalimbali wakati wa utekelezaji wa kazi yenyewe.



Moja ya changamoto ilikuwa ni baadhi ya wakimbizi kukataa kupanda mabasi  kwa kuhofia usalama wao huko waendako, hali iliyolazimu mbinu za ziada kuwashawishi kutumia.



Ili kuepuka machafuko, mkuu wa wilaya ya Kasulu Dany Makanga, viongozi na watumishi wengine wametoa raia kwa Watanzania kudumisha amani, utulivu na upendo miongoni mwao.



Wakizungumza  eneo la Musenyi nchini Burundi Lewisi Kisanja na John Claudio waliokuwa wakisubiri kwenda maeneo ya mikoa yao ya kuishi  wameiomba serikali yao ya  Burundi kuwalinda, kuwaendeleza kielimu na kuwapatia maeneo ya Kilimo.



Dotto Elias. TBC Kigoma.




Last Updated ( Thursday, 13 December 2012 11:33 )


 
Continuer la lecture

TANZANIE - accès rapides

Actualités par pays

 

Newsletter


 
 
 
 
 
 

Actualités par pays

Newsletter


 
 
 
 
 

Pub GOOGLE

Tanzanie - Actualites