PlaneteAfrique
Déconnexion

WS-Apps, Le système de gestion de contenu adaptatif développé depuis 15 ans est conçu pour sa puissance son efficacité et sa simplicité. WS-MySite! pour votre présence web immédiate, WS-Webzine pour vos publications, Ws-Ecommerce pour votre business.

Mwakyembe aagiza matrekta bandarini kutumika kwa kilimo

Publié le 8/5/2013
Mwakyembe aagiza matrekta bandarini kutumika kwa kilimo


Waziri wa Uchukuzi Dkt. Harrison Mwakyembe ametoa miezi mitatu kwa watu wote walioingiza matrekta nchini ya kifungu cha msamaha wa kodi ili kuboresha kilimo nchini, wahakikishe zana hizo zinatumika kwa kazi hiyo na siyo vinginevyo.



Dkt. Mwakyembe ametoa agizo hilo wakati wa uzinduzi wa Maonesho ya wakulima kwa nyanda za juu kusini yanayoendelea katika Viwanja vya John Mwakangale, huku akiagiza tabia ya kutumia matrekta kubeba na kukokota mizigo bandarini ikomeshwe mara moja na matrekta hayo yapelekwe mashambani kwa ajili ya kilimo.



Msimu wa maonesho ya wakulima na wafugaji umeanza, maonesho ya Nane nane kwa mikoa ya Kanda za Nyanda za Juu kusini yameshirikisha mikoa ya Njombe, Ruvuma, Katavi, Rukwa Iringa na Mbeya, mwaka huu maonesho haya yamezinduliwa na Waziri wa Uchukuzi Dtk. Harrison Mwakyembe.



Chama cha wakulima Nchini - TASO, Kanda ya Nyanda za Juu kusini kimepongeza hatua ya Waziri aliyofikia.



Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Njombe Kapteni Mstaafu Aseri Msangi amemhakikishia waziri mwaakyembe kuwa wako katika jitihada za kutumia vema ujio wa Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Songwe, uwe ni manufaa kwa wananchi wa mikoa ya Kanda ya Nyanda za juu kusini.



Hosea Cheyo, TBC Mbeya.




Last Updated ( Friday, 02 August 2013 09:11 )


 


Continuer la lecture

TANZANIE - accès rapides

Actualités par pays

 

Newsletter


 
 
 
 
 
 

Actualités par pays

Newsletter


 
 
 
 
 

Pub GOOGLE

Tanzanie - Actualites